Thursday, June 28, 2012

Analisha mbung'o

Chakula cha mbung'o ni damu. Hivyo mbung'o wanaofanyiwa utafiti kituoni TTRI-Tanga hulishwa damu ya wanyama (mbuzi au ng'ombe).Kutunza mbung'o wa utafiti ni zoezi gumu na ni gharama. Linahitaji umeme wa uhakika wakati wote, wafanyakazi wanaojituma na uangalifu wa hali ya juu. Kwani kosa dogo tu linaweza kusababisha mbung'o wengi kufa. Mbung'o wanaofugwa hutumika kitaalmu katika kutokomeza mbung'o wengine.Wananchi wengi hawajui kinachoendelea hapo kituoni na wengine hutua habari za uongo kuwa kituo hicho hushughulika na unyonyaji wa damu hiyo si kweli ni vizuri wananchi waweze kutembelea kituo hicho na kujionea wenyewe jinsi watafiti wetu wanavyoshughulika na utokomezaji wa mdudu hatari mbung'o ambao husababisha ugonjwa wa malale kwa binadamu na ndigana kwa wanyama hatimaye vifo.
Hawa ndiyo mbung'o wanaofugwa.

No comments: