Friday, June 29, 2012

Nguzo ya familia miaka 70

Mwezi wa sita 2012 shangazi yangu Paulina Ephrem Kibena (Mama Mloka) ametimiza miaka 70 akiwa na nguvu na afya tele. Bila kutegemea watoto wake Fredy, Doreen, Petty na Ceasar (The Mlokas) walimuandalia tafrija fupi ya kumpongeza. Shangazi Pau ni kiungo mkubwa kwa familia yetu. Wengi tumepitia kwenye malezi yake, ametusomesha na kutuozesha amefanya kuwa karibu na ndugu na jamaa wengine. Msimamo wake umesaidia sana kuijenga familia mahali ambapo ipo. Ninakupongeza sana shangazi yangu kwa kutimiza umri huo wa miaka 70 MUNGU akupe afya na maisha marefu zaidi. AMINA

No comments: