Tuesday, June 5, 2012

Majani ya Kaskasi

Kwenye maonesho ya NaneNane (Siku ya Wakulima)mwaka jana (2011) wakulima wa kutoka Kibungo JUU wilaya ya Morogoro Vijijini kwenye banda lao walionyesha matumizi bora ya ardhi.Moja ya teknolojia waliyoionyesha inayotumika kuhifadhi ardhi ni upandaji wa mmea unaoitwa kaskasi au kwa lugha ya Kiluguru 'usoti' (pichani) kuzuia mmomonyoko wa ardhi milimani. Licha ya kuhifadhi ardhi, kaskasi hutumika kuezeka nyumba.

No comments: