Friday, June 1, 2012

Wanamwita 'Mwabeshi'

Huyu anaitwa Shabani. Lakini hapa kijijini kwetu Kisemvule ni maarufu sana kwa jina la 'Mwabeshi' likiwa na maana ni mtu kutoka Ethiopia! Kwa maelezo yake mwenyewe ni kwamba, jina hilo amelipata hapo Kisemvule kwa kuwa alikuwa anafanya kazi kwa mtu aliyefananishwa na waethiopia lakini kumbe alikuwa ni mchangayiko wa damu ya kihindi na watu kutoka Tabora. Shabani kazi yake ni biashara ndogondogo hasa matunda kwa kuzingatia msimu kuna wakati anauza embe, kuna wakati mwingine machungwa. Hapa alikuwa anauza mahindi ya kuchoma. Huyo ndiye Shabani 'Mwabeshi' ameoa na ana watoto watatu

No comments: