Friday, June 29, 2012

Tanesco yatangaza neema


SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO) limetangaza kuwa wateja wote walioomba kupata huduma ya kuunganishiwa umeme kwa muda mrefu wanapaswa kuwa wameunganishiwa umeme ifikapo Juni 30 2012 kwani kwa sasa shirika hilo lina vifaa vya kutosha hayo yamesemwa na Msemaji wa Shirika hilo Bi Badra Masoud. "Hakuna mfaynyakazi wa Tanesco anayepaswa kumzungusha mteja hivyo mteja yeyote atakayezungushwa awasiliane na makao makuu ili waweze kushughulikiwa. Tutatoa namaba maalum ili wateja ambao watakuwa wanasumbuliwa na wafanyakazi wetu waweze kutupigia moja kwamoja na sisis tutashughulika nao," alisema.(Chanzo cha habari-Gazeti la Mwananchi 29/6/2012)

No comments: