Friday, June 29, 2012

Askofu Mtanzania kuongoza Idara ya Uinjilishaji Vatican


PAPA Benedict XVI amempandisha cheo na kumteua Askofu wa Jimbo la Kigoma wa Kanisa Katoliki, Protase Rugambwa kuongoza Idara ya Uinjilishaji akiwa pia Rais wa Baraza la Kipapa la Umisionari. Kwa uteuzi huo wa Juni 26, mwaka huu ambao ulitangazwa na Shirika la Habari la Kipapa, Fides Agenzia, Askofu Rugambwa sasa atakuwa na hadhi ya Askofu Mkuu. (Chanzo cha habari- Gazeti la Mwanachi 29/6/2012)

No comments: