Wednesday, June 27, 2012

Utafiti wa mbolea kwenye mahindi

Utafiti huu unafanyika wilayani Handeni kwa ushirikiano wa wakulima na watafiti wa kituo cha utafiti cha Mlingano kilichoko mkoani Tanga. Hapa tulipata maelezo kutoka kwa wakulima kuwa mbolea ya DAP imeonyesha matokeo mazuri ukilinganisha na mbolea nyingine. Jaribio halijafikia tamati. Watafiti watatuandikia kuhusu jaribio hili pindi watakapomaliza utafiti wao.

No comments: