Friday, August 3, 2012

Bodi ya VSS-Kikao cha I

Tarehe 30/6/2012 Bodi ya Vikindu Secondary School ilikaa kikao chake cha I na kumchagua Bw. Bakari Chande kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi. Mambo makuu yaliyozungumzwa katika kikao hicho ni kuhusu miundo mbinu ya shule hasa ubovu wa vyoo, upungufu wa viti na madawati kwa wanafunzi,mimba kwa wasichana na utoro sugu. Kuhusu tatizo la ubovu wa vyoo, wajumbe kwa pamoja waliamua kuchangia sh. 20,000/- kila mmoja na kuazimia kuitisha kikao na watendaji wa vijiji wa Kata ya Vikindu kuzungumzia matatizo yanayoikabili shule ya Sekondari Vikindu.

No comments: