Saturday, August 11, 2012

Nzige ni balaa

Nzige ni wadudu aina ya panzi ambao hushambulia mazao yakiwa shambani.Huzaliana kwa wingi na wakitua eneo la majani mabichi hushambulia kila kitu. Kupambana na nzige ni kazi rahisi zinahitaji umaja wa kimataifa kwani wadudu hawa huruka bila ya mipaka wanaweza kuzaliana Kenya na kutua Tanzania au Kongo na kuja kuharibu mazao nchini Tanzania. Kwenye maonyesho ya Nanenane 2012 kanda ya Kaskazini jijini Arusha,Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika ilikuwa na sehemu ambayo wataalamu wake walikuwa wanaelezea masuala ya nzige na jinsi Serikali inavyopambana na wadudu hao waharibifu.

1 comment:

Gaitan John said...

Shem unajua Novemba 3, 2012 tumempoteza Bibi yetu bint Mawenge ila tulipata changamoto kujua amezaliwa mwaka gani? Hatimaye kumbukumbu zilizopo ni kuwa bibi aliona nzige ya kwanza na ya pili. Sasa nikajaribu kusearch nikaona umeiweka hii kwenye blog yako pengine unaweza kutusaidia kujua hizo awamu mbili za nge zilikuwa ni miaka gani.