Saturday, August 11, 2012

Unaweza kuhifadhi kilo 400 za nafaka

Wadudu waharibifu hashanbulia mazao hata yakiwa shambani. Teknolojia nyingi zimebuniwa kudhibiti wadudu hao kama vile vifukusi na 'scania' wasishambulie mazao kwa kutumia madawa na njia nyinginezo. Lakini teknolojia hii ya ghala linalohamishika linaonekana kuleta ahueni kwa wakulima. Watafiti wa Kituo cha Utafiti Selian kanda ya Kaskazini wakishirikiana na CIMMYT wameanza kusambaza teknolojia hii kwa wakulima. Ghala la aina hiyo huuzwa kiasi cha shilingi 140,000/-. Ghala hili limeonekana kuwavutia wadau wengi kwenye maonyesho ya Nanenane 2012 katika viwanja vya Temi jijini Arusha.

No comments: