Tuesday, January 5, 2010

Bongo-Dar Es Salaam mbinu za wizi usipime

Wizi wa vyombo vya magari vinaenea kwa kasi jijini Dar Es Salaam. Wenye magari wanaibiwa, vioo, wind screens, mud guards na chochote kinachoweza kutolewa. Ukikitafuta utakipata Gerezani tena kile kile ulichoibiwa na utauziwa kwa bei mbaya. Lakini ole wako kama utajaribu kuchukua hatua hukipati. Hii ndiyo hali hali ya wizi wa vyombo vya magari jijini Dar.

Dar epuka kutoa lift kwa mtu usiyemfahamu ni hatari hata kama ataonyesha kukufahamu na kukutaja kwa jina kama uko peke yako ongeza mwendo. Mtu huyo anaweza kukuibia chochote kilichomo ndani ya gari (comupter,simu ya mkononi na vinginevyo) kundi hili la wezi liko pale njia panda ya Kilwa na Nelson Mandela kama unakwenda Uwanja wa UHURU.

Dar, usione mtu mzee tena mstaarabu amevalia kanzu na kofia (bargashia) ukafikiri ni muumini mzuri, mwanafunzi kavalia uniform yenye beji ya shuli pamoja na bag lake. Kaa chonjo anaweza kukutoa upepo mara moja ukiwa ndani ya daladala.

Dar usione umekaa kwenye kiti cha daladala na binti mrembo ukafikiri wote ni wasafiri. Kaa chonjo unaweza kushtukia huna pochi na simu haiko vilevile na binti alikoshukia ni kitendawili.Hii ndiyo Bongo Dar Es Salaam. Wakati tunaanza mwaka mpya tuwe makini.

No comments: