Friday, January 15, 2010

Mafuriko yaliyoikumba Kilosa Kusini yanatisha

Ukitokea Mikumi na kuingia Kilosa mjini hutaamini macho yako, sehemu kubwa imetota maji, tope. Unapoingia mjini na kupita barabara ya kwenda Ilonga kwenye shule ya msingi Mazinyungu na hospitali ya wilaya ya Kilosa unaona makundi ya watu, vitanda viko nje, madirisha , milango, mabati huku makundi ya watoto wadogo wanacheza na mahema yamejengwa kuhifadhi waathirika na mafuriko. Ni simanzi kubwa sana. Mafuriko yamewafikisha hapo walipo kwa kipindi kifupi bila kutarajia.

Mji wa Kilosa umefurika watu wa aina mbalimbali ili kuweza kurekebisha mambo. Nyumba za wageni hazitoshi na hata huduma za chakula nazo hazikidhi haja. Haya ndiyo matokeo ya maafa. Kweli maafa ya Kilosa yanasikitisha. Yameathiri watoto, wakubwa wazee, wake kwa wakulima yamerudisha nyuma maendeleo yao.

No comments: