Tuesday, January 26, 2010

Misri na Algeria wako mbali kisoka


Mimi ni mmoja wa mashabiki wa soka la kiarabu iwe Misri, Algeria, Tunisia na Morocco. Hawa jamaa wanajua mpira, wanacheza kwa malengo,uzalendo na wametulia. Wanajua sana kuusoma mchezo wa wapinzani wao.

Jana niliangalia kwa makini mchezo wa robo fainali kati ya Misri na Cameroon. Wamisri walishambuliwa sana, walianza kufungwa wao na kuelemewa na mipira mingi ya kona lakini walitulia na hatimaye kuweza kuifungisha virago Cameroon mabao 3-1.

Misri wanaye mwalimu wa siku nyingi mzalendo Hassan Shihata. Anawajua wachezaji wake anaongea kwa lugha moja isitoshe anaangaliwa vizuri! Watanzania tujifunze kutoka kwa waafrika hawa. Tusishabikie rangi ya ngozi wote tunacheza CAN na tupo barani Afrika! (Pichani-Zidan wa Misri akimtoka Alexander Song wa Cameroon - kwa hisani ya gazeti la mwananchi 26/1/2010)

No comments: