Friday, January 8, 2010

Daladala za Mwenge -Posta raha tupu


Kama kuna daladala zenye ustaarabu jijini Dar basi ni zile ziendazo Mwenge-Posta. Kwanza ni 'pamba' ile mbaya. Abiria wastaarabu, kondakta wasafi. Mwendo ni wa usalama. Ndani ya bus kuna vitenga vya kutupa uchafu. Hebu angalia hata wakati wakupanda basi wanapanda kwa ustaarabu kama vile wamepangwa huku konda akigani Mwenge-Posta! Mpaka raha. Big Up daladala za Mwenge-Posta. Sumatra hebu wapeleke wamiliki wa mabus wa njia nyingine wakajifunze kwa wenzao wa Mwenge-Posta.

No comments: