Friday, January 29, 2010

Kwa kandanda ya jana Misri wana nafasi kubwa yakuwa mabingwa ' AFCON'


Nimekuwa nikifuatilia mechi karibu zote walizocheza timu ya Misri 'Pharaos.' Kusema kweli ni wazuri. Kila idara imekamilika na wanacheza kitimu na mkakati wenye lengo. Wachezaji wanauwezo wa kumiliki mpira, kupiga chenga, kutoa pasi, mbio, stamina na mikikimiki ya mpira si haba wanaijua.

Kitendo cha kuidungua Algeria mabao 4-0 katika mchezo wa nusu fainali uliofanyika jana usiku nchini Angola katika kumtafuta bingwa wa 'AFCON' sio mchezo. Yameingia bila ubishi wowote. Pharao hawa wameshinda mechi zote tena wamezishinda timu ngumu. Timu tunazotegemea kutuwakilisha vizuri kwenye kombe la dunia ( wao hawamo). Kuna nini tena!
Kwa uwezo walionao shilingi yangu naiweka kwao. (Picha kwa hisani ya Website ya CAF)

No comments: