Tuesday, January 12, 2010

Soko Kuu la Morogoro bado chafu

Kila inaponyesha mvua, Soko Kuu la Morogoro ni uvundo. Linanuka.
Nipo hapa Morogoro kikazi. Leo mchana nilipata fursa ya kutembelea soko hilo ni matope, matope ,matope. Nilimuuliza ndugu yangu Fau Mizambwa. Eee bwana vipi hapa mbona hakuna mabadiliko? Kila mwaka hali ni ileile wakati mazao yanayouzwa hapa hasa matunda na mboga mboga ni vya kiwango cha hali ya juu. Lakini usafi ni duni sana. Ujue walaji wengi wa matunda wanaponunua embe au ndizi hawana muda wa kuosha kwa hali hii, homa ya matumbo na kipindupindu haviwezi kuepukika.

No comments: