Friday, January 15, 2010

Tufanye kazi kama wanajeshi

Leo asubuhi wakati blog hii ikisafiri kuelekea Morogoro mjini ikitokea Kilosa. Ilikutana na msafara mkubwa wa magari ya Jeshi la Wananchi Tanzania. Nadhani yalikuwa yakielekea Kilosa kulikotokea maafa. Naambiwa kuwa wanaenda kujenga daraja lililoendolewa kwenye mto Mkondoa.

Jeshi limepokea agizo na tayari wameanza kutekeleza wana vifaa, wana watu na nina imani kuwa wataitekeleza kazi hiyo kwa muda mfupi sana. Blog hii inajiuliza hivi kwanini tusiwe kama wanajeshi katika kufanya kazi zetu?

No comments: