Friday, January 29, 2010

HIVI NDIVYO GYAN ALIVYOSHANGILIA GOLI LAKE DHIDI YA NIGERIA


Wakicheza mpira wa kufundishwa na wenye mkakati wa ushindi, Ghana licha ya kuwa na wachezaji wengi majeruhi na vijana wameweza kuwaondosha wakongwe na jirani zao timu ya Super Eagels ya Nigeria kwa goli moja kwa nunge. Goli lililofungwa kwa kichwa katika dakika ya 20 na mshambuliaji hatari wa kimataifa Asomoah Gyan lilikuwa ni goli zuri.

Nigeria walijaribu kila njia kuweza kusawazisha matokeo na hatimaye kupata ushindi lakini pilika hizo zilitibuliwa na ngome imara ya Black Stars. Pengine wa kumlaumu zaidi ni Obafeni Martins wa Nigeria aliyekosa mabao mengi huku akitegemea zaidi guu lake la kushoto. Pichani Gyan akishangilia bao lake.(Picha kwa hisani ya Website ya CAF)

No comments: