Thursday, January 28, 2010

Hatuna mpango endelevu wa kudhibiti ombomba jijini


Hii ndiyo hali halisi. Ombaomba wanazidi kuongezeka jijini. Na si kweli kuwa wote wanaoomba ni walemavu hata kidogo. Wengi wamejenga tabia ya kuomba. Omba omba wamezagaa sehemu mbalimbali jijini hasa wilaya ya Ilala. Wanapatikana kwa winngi pale 'fire' na kisutu. Kibaya zaidi watoto wadogo hutumika katika shughuli hiyo ya kuomba huku wazazi (hasa kinamama) wakiweka makazi yao kandokando ya barabara. Hivi tumeshindwa kuandaa mpango endelevu wa kuwadhibiti ombaomba? (Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi 28/1/2010)

No comments: