Friday, January 15, 2010

Wengi hawakifahamu Chuo cha Taifa cha Sukari (NSTI)

Kwa kuwa kinajulikana kwa jina la Chuo cha Taifa cha Sukari wengi hufikiri kuwa chuo hicho hutoa mafunzo ya kutengeneza sukari tu. Hii si kweli. Blog hii ilipotembelea chuoni hapo hivi karibuni ilijionea mengi na kujifunza mengi.

Chuo cha Taifa cha Sukari (NSTI) kiko Ruaha karibu kabisa na kiwanda cha Sukari cha Kilombero (KI). Licha ya kutoa mafunzo ya aina mbalimbali na kuwa na miundo mbinu na mazingira ya kuvutia chuo hakifahamiki na wengi.

Baadhi ya mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu yanayotolewa chuoni hapo ni pamoja na ufundi wa umeme wa majumbani na viwandani, utengenezaji wa kompyuta, ukarabati wa magari na utengenezaji wa vipuri vya aina mbalimbali pamoja na udereva. Mafunzo ya utengenezaji wa sukari unalenga mahitaji ya nyumbani au familia pamoja na viwandani. Chuo pia hutoa mafunzo ya kujifunza.

Tofauti na vyuo vingine chuo hicho hupokea hata wanafunzi waliomaliza darasa la saba kwani wanaamini na wanayo mifano ya wanafunzi waliopitia chuo hicho wakiwa na elimu ya darasa la saba na kufanya vizuri kuliko wale wa kidato cha nne au cha sita. Tukitafute na tuwapeleke vijana wetu NSTI-Kidatu.

1 comment:

Anonymous said...

ikochuo form zimetoka