Tuesday, January 12, 2010

Watanzania tuache uvivu tuchape kazi

Ni kweli mvua zinazonyesha hivi sasa kuna baadhi ya maeneo hapa nchini zimeleta maafa makubwa. Lakini ni kweli pia kuna baadhi ya sehemu mvua zinazonyesha ni neema. Hivi karibuni nilisafiri kwa bus Dar hadi Korogwe na leo nimesafiri kutoka Dar hadi Morogoro huko njiani nimeona jinsi mimea ya mazao iliyowahi kupandwa ilivyostawi vizuri. Kwa vyovyote vile wakulima walio wahi kutayarisha mashamba mapema na kupanda mapema watavuna. Lakini sehemu kubwa haijalimwa. Kwa hiyo utashangaa kwanini hali iko hivyo. Je, hatuna mipango mizuri ya kilimo? Au ni uvivu tu. Mimi naamini kuwa iwapo ardhi hii tunayoichezea wataruhusiwa wageni kuwekeza tutaona maajabu na sisi kubakia vibarua. Watanzania tuache maneno mengi tufanye kazi kwanza. Pengine badala ya kilimo kwanza tuseme "KAZI KWANZA."

No comments: