Thursday, January 28, 2010

Morogoro mkungu shilingi elfu 3 Dar ndizi 5 miatano


Licha ya kusafirisha mikungu yake ya ndizi hadi sokoni Morogoro. Mkulima huyu anauza mkungu mmoja kati ya shilingi 2,500 hadi 3,000/- Kwa bei hii lini ataweza kujenga nyumba bora ya kisasa na kuona kuwa kweli kilimo kinalipa? Bei ya bati moja ni shilingi 16,000/- (gauge 30) atahitaji kwa wastani mikungu saba aweze kununua bati hivyo kwa nyumba ndogo inayohitaji mabati 30 itabidi auze mikungu 180. Kutoka shamba la ukubwa upi na kwa muda gani? Kwa bei hii kweli kilimo kinalipa?

Mfanyabiashara jijini Dar huuza ndizi tano kwa shilingo 500 kwahiyo akiwa na ndizi 1000 tayari amekuwa ameshaingiza shilingi 100,000/- Tafakari.

1 comment:

gassim said...

Ndugu John napenda kuuliza swali
maji ya kisima yanafaa kumwagilia miwa
Abdallah.