Tuesday, January 26, 2010

Uchaguzi una mambo eti Abood anasonga ugali!


Leo asubuhi nimeinyaka picha moja ya kejeli kwa waathirika wa mafuriko wilayani Kilosa. Picha hiyo yenye maelezo kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kutoka Mkoa wa Morogoro, Aziz Abood, akimsaidia kusonga ugali mmoja wa waathirika wa mafuriko... Hivi kweli kusonga ugali kunasaidia wahanga wa mafuriko au dhihaka tu. Hii ni mikikimikiki kuelekea uchaguzi 2010 tuwe macho na watu hawa. Morogoro fungueni macho mnawajua wa kuwachagua!

No comments: