Friday, January 15, 2010

Tuache kujenga nyumba za biskuti!

Nyumba nyingi zilizoanguka baada ya kukumbwa na mafuriko mjini Kilosa ni zile zilizojengwa mabondeni kwa matofali mabichi au zile zisizojengwa kwa msingi imara. Nyumba hizi wenyewe wanaziita biskuti. Kwani biskuti ikiwekwa maji tu huyeyuka. Ndivyo ilivyotokea Kilosa. Wengi wameachwa bila makazi. Hili ni fundisho kwa wote kuwa tunapojenga nyumba tujitahidi kujenga msingi imara ikiwezekana tujenge kwa mawe au matofali ya saruji.

No comments: