Tuesday, January 12, 2010

HUDUMA HII YA ABOOD BUS INAKERA

Tarehe 9 Januari nilisafiri kutoka Dar kwenda Morogoro kwa shughuli za familia. Nilifika kituo cha Ubungo saa 3.30 asubuhi. Baada ya kukata ticket ya mabus ya Abood niliarifiwa kuwa safari itaanza saa nne kamili. Jambo la kushangaza ni kwamba niliweza kusafiri saa 7.00 mchana. Kwa nini nasema huduma ilikuwa ni mbovu ni kwasababu inasemekana gari letu lilipata hitilafu njiani. Kwahiyo wale waliokata ticket nyuma yetu mabus yao yalipokuja waliandoka na kutuacha. Kwa kuwa sisi hatukuchagua bus ilikuwa rahisi tu kwa utawala kuamua kuwa bus litakalofika kwanza ndiyo waliotangulia kukata ticket wapate huduma hiyo. Ni baada ya wasafiri kulalamika ndipo utawala wa mabus hayo ulipoamua kutupa bus lililofuata baada ya mabus matatu kutuacha.

No comments: