Friday, January 15, 2010

Ifakara sasa inafikika kirahisi

Miaka ya themanini na kurudi nyuma ukiambiwa kusafiri kwenda Ifakara hasa wakati wa masika hiyo ni adhabu kubwa sana. Barabara ilikuwa mbaya kweli kweli. Kutoka Mikumi hadi Ifakara barabara ilikuwa ya udongo yenye makona mengi na madaraja ya hapa na pale. Gari nazo zilikuwa chache na zilikuwa katika hali mbaya. Kwa kweli wenye magari yao hawakuwa tayari kupeleka Ifakara.
Hali imebadilika kabisa hivi sasa. Juzi nilisafiri kwenda Ifakara na kuona sehemu kubwa ya barabara hiyo imejengwa kwa kiwango cha lami hivyo kurahisisha usafiri kutoka Mikumi hadi Ifakara. Si ajabu kuona gari ndogo (taxi) zikisafairisha abiria kutoka Mikumi hadi Ruaha kwa shilingi 2,000/= tu. Hii ni hatua kubwa ya maendeleo. Nina matumaini kuwa hadi kufikia mwaka 2012 sehemu iliyobaki itakuwa imekamilika kwa kiwango cha lami.

Ikumbukwe kuwa inakopita barabara hiyo ni maarufu kwa uzalishaji wa mazao mbalimbali ya kilimo. Kwa kuimarisha barabara hiyo kutaongeza chachu ya uzalishaji wa mazao kama mpunga,miwa, ndizi na mahindi.

No comments: