Tuesday, January 5, 2010

Usipotunza mbegu si mkulima


Si rahisi mkulima kula chakula chote alichovuna bila kutunza mbegu ya kupanda kwa msimu ujao. Kwa kawaida mbegu huchaguliwa iliyo nzuri kwa mategemeo ya kutoa mavuno mazuri. Kwa kuona hilo watafiti wa kituo cha Utafiti Naliendele kila mwaka huandaa maonyesho ya mbegu. Wakulima wa sehemu fulani hualikwa na kila mmoja huleta aina ya mbegu ya mazao anayozalisha. Maonyesho haya ni muhimu na huvutia wakulima wengi kwani kwa kupitia maonyesho haya wakulima wanaweza kubadilishana mbegu, kuuziana mbegu pamoja na kujifunza usatawishaji wa mazao hayo. Huu ni utaratibu mzuri. Hata nchini Msumbiji utaratibu kama huu hufanyika. Wakulima nao wanacho cha kuonyesha kwa hiyo watafiti na wakulima hubadilishana uzoefu. Pichani wakulima wa Msumbiji katika maonyesho ya mbegu. Angalia mbegu za kunde, bamia, mtama,karanga, mahindi, ufuta zote zimeltwa

No comments: