Tuesday, January 5, 2010

Teknolojia mbadala ya matumizi ya mkaa


Miti inakwisha kwa matumizi mbalimbali uchomaji wa mkaa ikiwa ni shughuli mojawapo inayomaliza misitu. Watu wengi hapa nchini hutumia mkaa kama nishati ya kupikia. Hata hivyo kutokana na miti kupungua bei ya mkaa hupanda kwa kasi sana. Naambiwa gunia la mkaa jijini Dar Salaam kwa sasa ni shilingi 25,000/- Bei hii kwa vyovyote vile ni ya juu kwa watu wenye kipato cha chini.

Kwa kuwa tatizo linaeleweka, watu wamekuwa wakibuni teknolojia mbalimbali kwa kupata mbadala wa mkaa. Mojawapo ni mchanganyiko wa takataka za karatasi vumbi la mbao mabaki ya miwa, majani kwa kuyamba kwenye vitonge vidogo vidogo kama mkaa. Uganda, Kenya na hata Tanzania wameshanza kutumia teknolojia hii mbadala ya mkaa na kuonekana kupendwa zana na watumiaji wake hasa kutokana na bei ndogo ukilinganisha na mkaa wa asili.

No comments: