Thursday, January 28, 2010

KISE KIDS yaiparua Mpera 3-0


Magoli matatu yaliyofungwa katika kipindi cha pili yameiwezesha timu ya KISE KIDS inayoundwa na vijana wadogo wa kijiji cha Kisemvule kilichoko wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani kuiliza timu ya Mpera. Mchezo huo ni moja ya mapambano ya ligi inayoendelea kijijini Kisemvule kwa sasa yenye lengo ya kumpata bingwa atakayezawadiwa zawadi kemkem na kutoa burudani kwa wakazi wa Kisemvule kijiji kinachokua kwa kasi katika kata ya Vikindu.

Akiongea na blog hii mwalimu wa soka wa timu hiyo Bw Abdallah Pembe amesema kuwa siri kubwa ya ushindi wa timu yake ni mazoezi pamoja na nidhamu. Mwenyekiti wa kijiji cha Kisemvule Bw. Shaaban Makuka ameahidi kuiwezesha timu hiyo ya vijana ili iweze kutoa wachezaji watakaounda timu ya kijiji cha KISEMVULE ambayo kwa siku za hivi karibuni imekuwa haisikiki sana.

Jumamosi iliyopita KISE KIDS a.k.a 'Watoto Wetu' iliwatoa kamasi baba zao -timu ya VETERANS kwa kuwafunga mabao 4-2 katika uwanja wa Kisemvule Magengeni.

Timu ya KISE KIDS imeanzishwa mapema mwaka huu na tayari imeshaanza kutoa upinzani mkali kijijini hapo na kuwa gumzo kwa wazee na vijana.

No comments: