Friday, August 1, 2008

Foleni ya Mbagala inasababishwa na ubinafsi wa madereva

Licha ya kuamka mapema ili kuweza kuwahi ofisini, leo nimejikuta nikikwama Mbagala Sabasaba takribani kwa saa moja kutokana na foleni ya magari iliyosababishwa na baadhi ya madereva kutofuata utaratibu wa kuendesha gari.

Magari mengi yalikuwa yanakatiza njia wanazojua wenyewe na kusababisha magari kufungana karibu kabisa na kiwanda cha nguo- KTM.

Hali hiyo iliendelea hadi walipojitokeza askari wa usalama barabarani na kuchukua hatua kali kwa wale madereva waliokatiza njia ikiwemo kuwanyang'anya funguo za gari. Kuna askari mmoja wa kike alinifurahisha sana pale aliposimama mbele ya gari lililotaka kuingia barabara kuu kwa makosa. Bila kusema chochote alimgandisha kwa muda mrefu na hata gari letu kufanikiwa kupita. Ndiyo maana nasema foleni ya Mbagala (Barabara ya Kilwa) inasababishwa na ubinafsi wa madereva.

No comments: