Saturday, August 2, 2008

Kamokerere-Kijiji cha Chacha Wangwe

Sijawahi kufika Musoma,Tarime husan kijiji cha Kamokerere. Sijawahi kumuona uso kwa uso marehemu Chacha Wangwe aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime. Lakini kwa takriban wiki moja sasa, kijiji cha Kamokerere kimekuwa maarufu kupitia vyombo vya habari kufuatia kifo cha Chacha Wangwe.

Kwanini Kamokerere? Chacha Wangwe alikuwa mmoja wa wabunge maarufu kwa hoja zake nzito akiwa bungeni. Aliwawakilisha ipasavyo wapiga kura wake wa jimbo la Tarime ingawa alikuwa si wa chama tawala, yeye alikuwa ni wa CHADEMA.

Marehemu Chacha Wangwe alipata ajali akiwa safarini kutoka Dodoma kuelekea Dar Es Salaam. Kwa kuwa kifo chake hakikutarajiwa, wengi walidhani kuwa kifo hicho kilikuwa ni cha kupangwa yaani aliuawa ndiyo maana wapiga kura wake hasa kutoka kijiji cha Chamokerere walipandwa jazba kutaka kufahamu sababu ya kifo hicho.

Lakini kwa mujibu wa habari kupitia televesheni na magazeti ya leo asubuhi baada ya uchunguzi wa kitaalamu kufanyika mbele ya mashahidi ya pande husika imebainika kuwa marehemu Chacha Wangwe alikufa kwa ajali ya gari na kupasuka fuvu na ubongo kumwagika. Apumzike kwa amani Chacha Wangwe.

No comments: