Wednesday, August 6, 2008

Usipofika Msamvu Makuti unakosa mengi

Ukipata bahati ya kutembelea mji wa Morogoro. Usipate shida, moja ya sehemu nzuri na za kupendeza na zenye kutoa huduma za uhakika za chakula na vinywaji ni Msamvu Makuti.

Msamvu Makuti ipo ndani ya kituo kikuu cha mabasi cha mji wa Morogoro. Inafikika kirahisi ukielekea Dodoma, Dar Es Salaam au Iringa. Msamvu Makuti imeweza kujijengea jina hasa kwa nyama choma, supu na mchesho!

Watoa huduma wa Msamvu Makuti ni vijana wachangamfu wake kwa waume na huwapokea wateja mara tu wanapokaribia milango ya banda hilo la Makuti lilioezekwa kiutamaduni.

Ifikapo usiku starehe ya muziki inapatokana na usafiri wa kurudi sehemu uliyofikia au nyumbani kwako ni "bwelele." Msamvu Makuti inatoa faraja kwa wasafiri wakati wote kwa huduma ya chakula na vinywaji. Ukiwa Msamvu Makuti unaweza kujinunulia matunda ya aina mbalimbali yanayopatikana mkoani Morogoro hasa ndizi ,machungwa, maembe na mananasi.

Uwapo Msamvu Makuti milima ya Uluguru inakukonyeza huku maji yakitiririka!

No comments: