Saturday, August 2, 2008

Nauli Mpya Utafiti wa kina haujafanywa

Jana tarehe 1 Agosti nauli za vyombo vya usafiri zimepanda nchini kote hasa kwa usafiri wa magari. Kupanda huku kwa nauli kumewafanya watanzania wengi kufikiri jinsi ya kufanya ili kuweza kukabiliana na kupanda huku kwa nauli.

Tatizo hili limejitokeza kwa kina zaidi jijini Dar Es Salaam hadi kufikia wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuandamana kwenda ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam ili kuonana na Mh. Kandoro wamueleze kukerwa kwao na uwezo walio nao wanafunzi.

Wafanyakazi wengi hasa wa kipato cha chini kuongezeka kwa nauli ni kero kwao. Wafanyabiashara wadodowadogo "wamachinga, mamantilie" nao ni pigo itabidi waongeze bei ya sahani ya wali au wapige panga kwa bei hiyohiyo ili waweze kupata faida. Bidhaa feki nazo zitaoongezeka madukani.
Nasema utafiti haujafanyika kwa nauli mpya za sasa.

No comments: