Wednesday, August 27, 2008

WANAENDESHA NA KUYAACHA KIGAMBONI

Wakati Ujenzi wa Barabara ya Kilwa ukiendelea. Wenye magari kutoka Mbagala na vitongoji vyake huamua kupitia Kigamboni ili kukwepa foleni ya magari kwenye barabara hiyo wakati wa asubuhi. Hali inakuwa mbaya wanapotaka kuvuka kwa kutumia pantoni. Kunakuwa na msururu mrefu wa magari. Kutokana na hali hiyo wengi wao huamua kuyaacha magari yao Kigamboni na kupanda pantoni. Hii imekuwa biashara nzuri kwa walinzi waliopo maeneo ya kivukoni gari dogo hulindwa kwa kiasi kisichopungua shilingi 500. Blog hii ilishuhudia hali hii leo asubuhi.

No comments: