Thursday, August 14, 2008

Mafuta ya Alizeti yang'aayo

Kwa wale waliotembelea banda la Kilimo la Halmashauri ya Sumbawanga kwenye uwanja wa John Mwakangale Mbeya na kukutana na wakulima wa Laela, nadhani watakubaliana nami kuwa moja ya vivutio vikubwa kwenye banda hilo lilikuwa ni mafuta ya alizeti.

Mafuta hayo yalizutia wadau wengi. Baadhi ya wadau walipenda kufahamu, kwanini mafuta mengine ya alizeti yanayotayarishwa kienyeji huwa na harufu mbaya na hayana mvuto (kwa rangi). Mkulima wa Laela alijibu kuwa hii inatokana na jinsi yanavyotayarishwa. "Yakitayarishwa vibaya ni kweli huwa yanakuwa na harufu mbaya." Alikiri mkulima huyo. Mafuta hayo ya alizeti yaliuzwa kwa bei ya shilingi (T) 2500/= kwa lita moja.

Kilimo cha alizeti ni maarufu mkoani Rukwa, kama wakulima watapata mitaji ya kutosha inawezekana kuwaondolea umasikini kwa kuwaongezea kipato chao.

No comments: