Thursday, August 21, 2008

Mchakato wa kupata mikopo ya kilimo ina vikwazo vingi

Wakulima James Kyandarora, Bi Salma Mlwilo na Bw.Godwin Manase kwa pamoja wanakiri kuwa kilimo kimeweza kuboresha maisha yao kwa kuweza kujenga nyumba bora, kununua zana za kilimo, kununua baiskeli na kusomesha watoto (baadhi hadi chuo kikuu). Hawa ni wakulima wa mpunga kutoka Mbarali kupitia SACCOS ijulikanayo kwa jina la "RWANDA MAJENJE SACCOS." Wakulima hawa walishiriki kwenye maonyesho ya Nane Nane ya mwaka huu kwenye uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya.

Wakulima hawa hujishughulisha zaidi na kilimo cha mpunga ambacho uzalishaji huweza kufikia kilo 2500 kwa hekta moja. Tatizo kubwa la uzalishaji wa mpunga ni upatikanaji wa maji kwa wakati pia mchakato wa kupata mikopo ya kilimo ina vikwazo vingi walilalamika wakulima hao.

No comments: