Tuesday, August 12, 2008

Tujifunze kwa Wachina

Michezo ya Olimpiki inaendelea huko Uchina. Wengi hawakutarajia kuwa Wachina wangeweza kuandaa michezo hiyo kwa kiwango cha hali ya juu hasa wazungu wa Ulaya ya Magharibi na Wamarekani. Lakini tumeona jinsi ufunguzi wa michezo hiyo ilivyofana huko Beijing. Angalia halaiki yao, angalia ubunifu wao kwa kweli ni "excellent" hata hao tunaowaita wazungu walibaki kupiga makofi na kushangaa. Watu wa marika yote walishirikishwa, wa jinsi zote walishirikishwa. Lugha waliotumia ilikuwa ni ya Kichina na kila kiongozi wao alipoongea wao walishangilia. Walishangilia kwa kuwa walielewa, walshangilia kwa kuwa walikuwa wazalendo. Kwa kweli Wachina wanaweza,wanajitegemea na ndiyo maana wanakuwa tishio katika dunia ya leo. Kweli Watanzania inatupasa kujifunza kutoka kwa wachina.

No comments: