Thursday, August 14, 2008

Kalalu aina mpya ya mbegu ya Mpunga

Watafiti wa Kilimo wa Taasisi ya Utafiti Uyole wameweza kutoa aina mpya ya mbegu ya mpunga ijulikanayo kwa jina la Kalalu. Mbegu hiyo ilitolewa rasmi mwaka 2005.

Jina la mbegu hiyo limetokana na Mkuu wa wilaya ya Kyela aliyewahi kufanya kazi kwenye wilaya hiyo ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kuhimiza na kusimamia kilimo Mh. Mama Kalalu.

Sifa ya mbegu hiyo ni uvumilivu wa ugonjwa wa "Yellow Mottle Virus", hutoa mavuno tani 5 hadi 6 kwa hekta.

Mpunga ni zao maarufu kwa chakula na biashara wilayani Kyela.

No comments: