Thursday, August 14, 2008

Acheni vifuto,pensili, calculators na rula

Mkufunzi Mwandamizi wa Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (ICT) wa VETA - Morogoro amewataka wahasibu na maafisa ugavi wa Idara ya Utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kuachana na matumizi ya vifuto, kalamu za risasi, rula, na calculators kwani shughuli hizo sasa zinafanywa na kompyuta.

Aliyasema hayo wakati akitoa mafunzo ya ICT ya muda wa juma moja mjini Morogoro. Mkufunzi huyo alisema kuwa programu ya Microsoft Excel inaweza kuwatatulia matatizo ya wahasibu na maafisa ugavi katika kutayarisha taarifa mbalimbali zinazohusu fani yao kwa ufanisi zaidi iwapo wafanyakazi hao wataielewa vizuri na kuitumia katika kazi zao za kila siku.

Moja ya sifa za programu ya excel ni kurahisha katika kufanya mahesabu, kutengeneza majedwali na chart mbalimbali. Zaidi ya wataalamu 40 wanaendelea na mafunzo hayo yanayotarajiwa kumalizika tarehe 17 Agosti 2008. Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika chini ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP)

1 comment:

Innocent John Banzi said...

kweli banzi. Nasisi tumezidi kubeba calculator! Vifuto, correcting fluid. Aa excel kiboko