Thursday, August 21, 2008

K.F.HANSEN KUTOKA DENMARK HADI MBARALI

Maonyesho ya wakulima maarufu kwa jina la Nane Nane yaliyofanyika kwenye uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya mwaka huu (2008)uliwashirikisha wadau wengi. Mmoja wa wadau aliyepata bahati ya kuzungumza na blog hii ni mzungu K.F.Hansen wa asasi isiyo ya serikali ijulikanayo kwa jina la SOK iliyoko Mbarali. Asasi hii hujishughulisha zaidi na uuzaji wa pembejeo za kilimo hasa madawa na mbegu kwa ajili ya uzalishaji wa mbogamboga na matunda. SOK ilianza shughuli zake mwaka 2000.

Kwa mujibu wa Bw. Hansen, wakulima wa Tanzania wanakabiliwa na matatizo makubwa ya ukosefu wa pembejeo na elimu ya kilimo bora, aidha bei za mazao ya kilimo hailipi. Gharama za uzalishaji ni kubwa kuliko za kuuzia. Hansen anatambua kuwa wakulima wengi ni wadogowadogo. Zana za kilimo pia hazipatikani kwa urahisi lakini anakiri kuwa sasa kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo kuhusu upatikanaji wa pembejeo na zana za kilimo. Hansen amekuwepo nchini Tanzania tangu mwaka 1985 anazungumza kiswahili kwa ufasaha na kwa kweli anafahamu matatizo ya wakulima.

No comments: