Tuesday, August 12, 2008

Kwa huduma hizi hatuwezi kuendelea

Nipo mji kasoro bahari (Morogoro). Hali ya hewa si mbaya kwa kweli. Nimekuja kwa shughuli za kikazi. Kuna mafunzo ya teknolojia ya mawasiliano (ICT) inayoendelea hapa VETA Morogoro kwa wahasibu na maafisa ugavi wa Idara ya Utafiti na Mafunzo - Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. Wakati wa mapumziko washiriki wanapata chai na chakula. Lakini watoaji huduma ni goigoi, wakielezwa wananuna. Hawana ahadi za uhakika. Wanaweza kukueleza kuwa chakula kitakuwa tayari baada ya dakika tano kumbe ndo kwanza ugali unasongwa! Hivi kwa huduma ya aina hii tunaweza kuendelea? Lakini wanaotua huduma hii sio VETA Morogoro, bali kuna mjasiriamali moja ambao watendaji wake wanamuangusha. Kwa mwenendo huu kweli tutaendelea?

No comments: