Sunday, August 10, 2008

Licha ya lumbesa kupigwa marufuku - Wakulima bado wananyonywa


Hivi karibuni serikali ilipiga marufuku mtindo wa kufunga magunia ya mazao kwa mtindo wa"lumbesa" kwa sababu mtindo huo ulikuwa unawaibia wakulima.

Safari yangu ya Mbeya kwenye sherehe za nane nane nilibahatika kuongea na mkulima mmoja kuhusu agizo hilo je kwa wakulima lina manufaa yoyote? Mkulima huyo ambaye ni mwanamama alinijibu kwa kusema kuwa kwa sasa hali imekuwa mbaya zaidi.
Alitoa mfano kuwa yeye ni mkulima wa viazi mviringo. Kwa mtindo wa "lumbesa" alikuwa akiuza sh.42,000/= (Bei ya mwaka jana). Lakini sasa ujazo wa kawaida anauza kwa sh. 15,000/=. Kutokana na hali hiyo wanaibiwa sana na mkulima hapati chochote.

No comments: