Tuesday, August 5, 2008

Msamvu - Morogoro "Keep left" Kikubwa Tanzania

Nimebahatika kutembelea mikoa mingi hapa Tanzania lakini sijapata kuona "keepleft" kubwa na inayotunzwa vizuri kama ile ya Msamvu, Morogoro. "Keep left" hiki kiko kwenye makutano ya barabara ya morogoro, Iringa na Dodoma kwa kweli ni kikubwa. Kinachofurahisha zaidi ni jinsi Manispaaa ya Morogoro inavyokitunza. Kina maua mazuri ya aina mbalimbali na uhudumiwa vizuri kwa kumwagiliwa maji na kuondoa magugu yasiyohitajiwa. Sasa naweza kusema kuwa " Keepleft" cha Msamvu ni nambari wani hapa Tanzania. Aliyeona kikubwa zaidi ya hicho akitaje basi!

No comments: