Wednesday, August 27, 2008

Si YANGA

Ukiwa ndiyo mara yako ya kwanza kuingia jijini Dar Es Salaam. Na mara yako ya kwanza kutembelea maeneo ya Buguruni, karibu kabisa na Makao Makuu ya chama cha CUF kuna jengo dogo hivi lililopakwa rangi za njano na kijani na kuandikwa kwa herufi kubwa YANGA nafikiri utajiuliza je hayo ndiyo makao Makuu ya Klabu ya Dar Es Salaam Young Africans al maarufu -YANGA? Usidanganyike, hicho ni kitawi kidogo tu cha Yanga cha Buguruni. Makao Makuu ya Yanga yako Jangwani, ndo maana wanaitwa watoto wa Jangwani!

Lakini nyie Yanga wa Buguruni, kwanini msiandike Yanga Tawi la Buguruni? Mnawapotosha wananchi.

No comments: