Wednesday, August 27, 2008

MV ARINA Reggae tu!

Moja ya boti zinazovusha abiria na magari pale Kigamboni Kivukoni ni MV ARINA. Ukipanda boti hiyo hukosi kuburudishwa na muziki kupitia kwa vipaaza sauti vya kizamani-mono (vya kutangazia mikutano). Lakini cha kushangaza, kama alivyobaini msafiri mmoja wa boti hiyo kwamba "humu hakuna taarifa ya habari wala nini - Ni Reggae tu." Hakufahamu kuwa blog hii ilikuwa karibu naye na pia huwa inatumia MV ARINA mara kwa mara na kusikia muziki wa reggae tu. Kweli MV ARINA ni reggae tu.

No comments: