Wednesday, August 13, 2008

Ludewa imepiga hatua kwa shamba darasa

Wakati wa sherehe za nane nane mwaka huu, banda la Halmashauri ya Ludewa lilikuja na takwimu nzuri za kuonyesha jinsi wakulima walivyopokea "approach" ya shamba darasa katika kujifunza teknolojia bora za kilimo.

Taarifa inaonyesha kuwa shamba darasa lilianza kutekelezwa kwenye Halmashauri hiyo tangu mwaka wa fedha 2005/06. Mwaka huo kulikuwa na mashamba darasa 13 ambayo 8 yalikuwa ya mazao na 5 mifugo. Mwaka 2006/07 kumekuwa na mashamba darasa 35 . Kumi na tisa ya mazao na kumi na sita ya mifugo. Kwa msimu wa mwaka 2007/08 kumekuwa na mashamba darasa 40 ambayo 22 ni mazao na 18 ni mifugo. Kwa takwimu hizo inaonyesha kuwa Ludewa inaendelea vizuri na shamba darasa.

Akizungumza na blog hii, Bw. Luoga aliyewakilisha Halmashauri katika maonyesho hayo, yaliyofanyika kwenye kiwanja cha maonyesho ya kilimo cha John Mwakangale kilichopo Uyole Mbeya(Kanda ya Nyanda za Juu Kusini), mtaalamu huyo wa kilimo alisema kuwa, wanawake wanaongoza kwa kupokea haraka "approach" ya shamba darasa lakini sasa wanaume wengi hujiunga na mashamba darasa ili kuweza kujifunza teknolojia mbalimbali za kilimo na ufugaji bora.

No comments: