Wednesday, August 27, 2008

Tumekula machungwa mwaka mzima wabunge tusubiri maembe

Wakulima wa nchi hii wanafanya makubwa ya kulisha watu waishio hapa nchini kwa vyakula mbalimbali na katika mazingira magumu. Licha ya gharama za juu za uzalishaji. Lakini bado hawsiti kuzalisha.

Mwaka huu nimeshuhudia machungwa yakiliwa jijini Dar kwa mwaka mzima sasa.Tembelea masoko ya Buguruni, Tandika na Mbagala machungwa matamu makubwa yapo kwa bei ya shilingi 100 kwa chungwa.

Machungwa haya yanazalishwa kwa kutegemea mvua, yanazalishwa bila mbolea, yanazalishwa bila kutumia viuatilifu. Machungwa bora kabisa. Yanaweza kupata soko zuri ndani na nje ya nchi. Wakulima wetu wanajitahidi sana. Rais wetu Mh.Jakaya Kikwete analifahamu hilo ndiyo maana kama kiongozi wa nchi aliamua kuwa fedha za EPA zinazorudishwa zipelekwe kwenye sekta ya kilimo ili ziwasadie wakulima. Hapa hakuna sababu ya wabunge kupanga. Kazi ya kupanga ni ya serikali wabunge kazi yao kupitisha tu. Asante sana Spika wa Bunge Mh. Samwel Sitta kwa kulifafanua hilo, vinginevyo nalo lingetusumbua. Wabunge tusubiri maembe.

No comments: