Monday, August 25, 2008

Usafiri Mtoni Mtongani-Mbagala ni kero tupu

Barabara ya Kilwa iko kwenye ujenzi mkubwa. Awamu ya pili imeanza na kazi inakwenda kwa kasi kwa kweli. Sambamba na ujenzi huu, usafiri kwenye barabara hiyo umekuwa wa shida sasa. Madaraja yanayojengwa (mto Kizinga) pamoja na uzikwaji wa makalavati yanafanya kuwe na michepuko ya barabara hapa na pale kiasi cha kupunguza mwendo wa magari na kusababisha msururu mrefu wa magari. Ubadilishaji wa nguzo za umeme nao huenda sanjari na ujenzi wa barabara. Miti hukatwa na mitaro kuchimbwa. Hapo ndipo shughuli inapokuwa kubwa. Unaweza kutumia masaa mawili hadi matatu kufika mahali ulipokusudia. Tatizo ni kubwa wakati wa jioni na asubuhi.

No comments: