Saturday, August 16, 2008

Kuiona Black Stars Tshs 35,000 hivi tunamkomoa nani?

TFF imetangaza viingilio vya mechi ya Black Stars ya Ghana na Taifa Stars huku kiwango cha juu kikiwa shilingi 35,000. Mchezo huo utakaochezwa kwenye uwanja mkuu wa Taifa Agosti 20. Hivi hapa tunajifunza nini? TFF haijawahamasisha wananchi kuhudhuria mchezo huo wa kirafiki. La msingi kwao ni kutangaza viingilio. Huku wakiweka wazi kuwa gharama ya kuileta Black Stars ni shilingi 175,000,000.

Kwa uelewa wangu Black Stars wanakuja kucheza na Taifa Stars ili kuweza kuipima timu yetu ya Taifa na ikiwezekana kujifunza kutoka kwa Waghana hao kwani tunaaamini kuwa kiwango chao cha soka ni kikubwa ukilinganisha na cha kwetu, pia wana wachezaji wengi wenye uzoefu wa kimataifa. Sasa tunapoweka viingilio vya kukomoa, tunamkomoa nani?

No comments: