Thursday, August 14, 2008

Ngano aina ya Sifa "bomba" kwa mkate

Mbegu ya ngano ijulikanayo kwa jina la Sifa iliyotolewa na watafiti wa Kilimo wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Uyole mkoani Mbeya ni moja ya aina nzuri ya ngano inayofaa kwa kuoka mkate.

Mbegu hiyo yenye sifa ya kukomaa kwa muda wa siku 105 (miezi 3). Ni tegemeo kubwa kwa wakulima wa wilaya za Njombe(Iringa), Sumbawanga Vijijini na Nkasi (Rukwa).

Aina hiyo ya ngano ilionyeshwa kwenye maonyesho ya wakulima yaliyofanyika mwaka huu jijini Mbeya kwenye uwanja wa John Mwakangale. Mtafiti Mkuu Elanga ilidai kuwa pamoja na kuwa na aina mbalimbali za mbegu bora za ngano zilizozalishwa na Taasisi hiyo bado hazijasambazwa kwa wakulima wengi.

No comments: